Wavuvi wa kinyume na
sheria
12/03/2009

Wavuvi wa kinyume na sheria ambao wapatao
38 wamefikishwa mahakamani kwa tuhuma ya uvuvi wa kinyume na sheria
katika bahari ya hindi ya Tanzania.

Wavuvi hao ambao walikuwa na chombo cha
meli inayoitwa Tawariq I ilikamatwa katika operesheni maalum
iliyoshirikisha mabaharia kutoka Tanzania, Afrika Kusini, Msumbiji na
Kenya. Meli hiyo ilikamatwa katika siku ya pili ya operesheni maalum
iliyoanzishwa na Tanzania kukomesha wizi wa samaki katika eneo lake la
Bahari ya Hindi.
Tanzania, Kenya na Msumbiji zimetoa mabaharia wawili-wawili na Afrika
Kusini imetoa mabahari watano. Rais Kikwete alitoa shukrani alipokutana
na mabaharia waliofanikisha kukamatwa kwa meli hiyo kubwa.
|