Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Tanzania hatarini kukosa rubani Mzalendo

19/03/2009

Kutokana na rubani wengi kuzeeka wa Tanzania, Tanzania inaweza kujikuta haina hata rubani mmoja mzalendo katika miaka mitano ijayo. Kutokana na hali hiyo, serikali imeshauriwa kuweka mkakati kamambe wa kutoa mafunzo kwa marubani wengi zaidi ili kuepuka aibu hiyo.

Ushauri huo ulitolewa juzi jioni na Mohamed AbdulKarim, ambaye ni Mwenyekiti wa Shirikisho la Utalii Tanzania, wakati akichangia kwenye mkutano wa wawekezaji wa ndani ulioandaliwa na Baraza la Taifa la Biashara (TNBC).

Abdulkarim alisema inapendeza zaidi iwapo ndege za Tanzania zitakuwa zinarushwa na marubani na wahudumu wazalendo. "Kuwa na ndege za serikali kunaleta maana zaidi iwapo kutakuwa na marubani na wahudumu wazalendo na hata vyakula vya Kitanzania ikibidi viwepo," alisema.

Pia, alisema wakati Tanzania inapata Uhuru ilikuwa na rubani mmoja hali iliyolazimu nchi za Afrika Mashariki kuanzisha mkakati wa kufundisha marubani na wahandisi wa ndege. Alisema watu kumi kutoka Afrika Mashariki walikuwa wakipewa mafunzo kila mwaka hadi jumuiya hiyo ilipokufa mwaka 1977.

Abdulkarim alisema hata baada ya kuvunjika jumuiya hiyo, Serikali ya Uganda yenyewe iliendelea na mkakati wa kufundisha marubani wazalendo. Aliendelea kusema kuwa serikali lazima iwe na mkakati huo wa kugharamia mafunzo kwa marubani kwa maslahi ya nchi kwa kuwa, watu wa hali ya chini hawawezi kumudu gharama za mafunzo hayo.

Alisema kuna wakati Tanzania ilikosa kabisa marubani na ililazimika kutumia wale waliokuwa jeshini. "Marubani hawatoshi na waliopo wamezeeka hivyo lazima tuwe na mkakati thabiti wa kufundisha watanzania urubani".

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©