Mgao wa umeme waanza Dar
es Salaam
29/03/2009

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limetangaza rasmi
mgawo wa nishati ya umeme kwa Mkoa wa Dar es Salaam kutokana na kupungua
kwa ufuaji wa umeme kwa megawati 50. Taarifa iliyotolewa leo na Tanesco,
ilisema mgawo huo wa muda utakuwa ni wa kila siku kuanzia saa 4 asubuhi
hadi saa 8 mchana na saa 12 jioni hadi saa 4 usiku.
Hali hiyo, taarifa ilisema imechangiwa na kusimama kwa
mitambo miwili katika kituo cha Songas (UGT1 na UGT5) ambacho kwa
kawaida huzalisha megawati 53. Mmoja unafanyiwa ukarabati wa kawaida na
mwingine umeharibika. Ilisema usambazaji umeme kwa Dar es Salaam na
Zanzibar unategemea nishati hiyo kutoka mitambo ya nguvu za maji na
mtambo wa gesi wa Ubungo kupitia transfoma namba T6 na T7. Pichani juu
ni makao makuu ya umeme nchini TANESCO iliyopo Ubungo jijini Dar es
Salaam.

|