Meli yakwama bandarini
01/04/2009

Meli ya mizigo ya MSC Federica iliyokwama jana jioni
katika eneo la Feri ya Kigamboni baada ya kutokea matatizo kwenye
usukani na kushindwa kukata kona. Meli hiyo ilikuwa inatokea katika
Bandari ya Dar kuelekea nchi za nje. Juhudi za kuikwamua zinaendelea
ikiwa ni pamoja na kupunguza maji na mafuta kwenye meli ili kupunguza
uzito.

Meli ya MSC Federica imekwama kwa siku ya pili baada ya
kuingia pembezoni mwa pwani ya Kigamboni. Inasemekana kuwa bado kidogo
tu kuvamia soko la kimataifa la Ferry lakini limekoswa kwa jitihada za
nahodha wa meli hiyo.
|