Bili za ZAIN kwa njia ya
ATM
05/04/2009

Meneja Mauzo na Uzalishaji wa Stanbic Bank, Lilian
Kitomari (katikati) akiwaonyesha waandishi wa habari jinsi wateja wa
Zain wanavyoweza kulipia bili zao za simu na kuongeza muda wa maongezi
kupitia ATM za Stanbic wakati wa uzinduzi wa huduma hiyo, jijini Dar es
Salaam. Kushoto ni Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Stanbic, Abdallah
Singano na kulia ni Meneja Masoko wa Zain Tanzania, Costantine Magavilla.
|