Wakimbilia Mafuta,
ajalini Morogoro
06/04/2009

Wakazi wa eneo la Misheni, nje kidogo ya mji wa Morogoro,
wakigombea mafuta yaliyokuwa yakimwagika kutoka kwenye tenki
lililoanguka mahali hapo wikiendi ilopita. Pamoja na kuwepo polisi wa
usalama barabarani mmoja aliyekuwa akijitahidi kuwafukuza wakazi hao,
wananchi walikuwa wabishi na kutoogopa lolote ambalo lingetokea la
kuhatarisha usalama wao.

Baada ya lori la mafuta kuacha tela lake likijiendesha
lenyewe baada ya kuchomoka na kuingia porini, al manusra ifinyange
finyage hii gari aina ya Escudo ilioacha njia kwa kulikwepa lile tela
lililokuwa limesheheni mafuta ya taa.

Baadhi ya wakazi wa eneo la Misheni wakiwahi kusitiri
mafuta ya dezo baada ya kuitika mbiu ya ajali hiyo!

Escudo iliponea chupuchupu kusombwa na roli la mafuta
lilolokuwa likienda adijojo.

End zis iz Jeki Cheni
staili. Cha kuokota si cha kuiba...
|