Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

JK mgeni rasmi katika hafla ya 40 ya Mzee Mloo

07/04/2009

JK akitoa hotuba yake wakati wa kumuombea Dua Marehemu Mzee Shaaban Khamis Mloo iliyofanyika katika ukumbi wa hoteli ya Lamada jijinji Dar es Salaam jioni ya tarehe 04/04/2009. Kulia ni Mwenyekiti wa Chama Cha CUF Profesa Ibrahim Lipumba na kushoto ni Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif Shariff Hamad.

JK akijadiliana jambo na Mwenyekiti wa CUF Profesa Ibrahim Lipumba na katibu Mkuu wa Chama hicho Seif Shariff Hamad wakati wa hafla ya kumuombea Dua Marehemu Mzee Shaaban Khamis Mloo ambaye ni mmoja wa waasisi wa Chama cha CUF. Hafla hiyo ilifanyika katika ukumbi wa hoteli ya Lamada jijinji Dar es Salaam ambapo JK alialikwa kama mgeni Rasmi.

JK akiwa na Mwenyekiti wa Chama Cha CUF Profesa Ibrahim Lipumba (kushoto) na Katibu Mkuu wa CUF Seif Shariff Hamad wakitoka nje ya ukumbi wa mikutano wa Hoteli ya Lamada jijini Dar es Salaam baada ya dua ya kumuombea marehemu Mzee Shaaban Khamis Mloo aliyefariki hivi karibuni. Mzee Shaaban Khamis Mloo alikuwa mmoja wa waasisi wa CUF. Rais Kikwete alialikwa kuwa mgeni Rasmi katika hafla hiyo.

Kwa vicheko na madaha, viongozi wa vyama viwili vya Tanzania wamekutana katika tukio ambalo limeondoa tofauti zao, hiyo ndio Tanzania tunayoijua.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©