KARUME DAY - kumbukumbu za
Rais Abeid Amani Karume
08/04/2009

Tarehe
07/04/2009 ilikuwa ni siku ya KARUME DAY ambayo kila mwaka tarehe na
mwezi huo hufanyika kumbukumbu ya Rais Abeid Amani Karume. Pichani juu
ni ukumbusho wa waasisi wa taifa hili la Tanzania, Mwalimu Nyerere na
Sheikh Abeid Karume, walipotembelea Ngome Kongwe huko Zenj enzi hizo.
Mwenye kanzu ni Sheikh Thabit Kombo.

Baadhi
ya Wananchi wa Zanzibar walohudhuria maombolezi ya Kumuombea Rais wa
Kwanza wa Zanzibar Marehemu Mzee Abeid Amani Karume iliyofanyika katika
ofisi kuu ya CCM Kisiwandui, Zanzibar katika kuadhukisha Karume Day.

Viongozi wa
Kitaifa akiwemo JK, Rais wa Zanzibar Amani Abeid Karume, Makamu wa Rais
Dr. Ali Mohamed Shein wakishiriki katika maombolezi ya kumuombea dua
njema Rais wa Kwanza wa Zanzibar na Muasisi wa Muungano wa Tanganyika na
Zanzibar Marehemu Abeid Amani Karume, katika kaburi lake lililopo nje ya
jengo la Ofisi kuu ya CCM, Kiswandui, Zanzibar. Dua hiyo ni sehemu ya
maadhimisho ya siku ya Karume Day ambayo huadhimishwa kila mwaka
kumkumbuka na kumuombea kiongozi huyo aliyeuawa kwa kupigwa risasi siku
ya tarehe 07/04/1972.

Mjane wa
Rais wa Kwanza wa Zanzibar, Marehemu Abeid Amani Karume, Mama Fatma
Karume (katikati) akiwa pamoja na mke wa Rais wa Zanzibar Mama Shadya
Karume (kushoto) pamoja na mke wa Makamu wa Rais Mama Mwanamwema Shein
wakishiriki katika dua ya kumuombea muasisi iliyofanyika katika Kaburi
lake lililopo katika jengo la ofisi kuu ya CCM, Kiswandui, Zanzibar.

Viongozi
wa madhehebu mbalimbali ya dini walishiriki katika dua ya kumuombea
marehemu Abeid Amani Karume katika kaburi la muasisi huyo huko
Kisiwandui, Zanzibar.

JK akiwa
katika mazungumzo na Rais wa Zanzibar Amani Abeid Karume, ikulu mjini
Zanzibar mara baada ya maadhimisho ya Karume Day yaliyofanyika Zanzibar
tarehe 07/04/2009.

JK
akiagana na Rais wa Zanzibar Dk. Amani Abeid karume baada ya kuhudhuria
shughuli za Karume Day Zanzibar.
|