Bi Salma mgeni wa heshima
SACOSS - Zanzibar
13/04/2009

Mwenyekiti wa WAMA Mama Salma Kikwete akimkabidhi Mweka hazina wa SACCOS
ya Meli Nne, Bi Shamsa Saleh Hilal, mchango wa Shilingi Milioni Tano
5m/- kutoka kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda wakati wa hafla ya ufunguzi wa
Mkutano Mkuu wa Tatu wa SACCOS uliofanyika katika Chuo cha Karume,
Mwanakwerekwe, Zanzibar. Kulia ni Waziri kiongozi wa Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar Mheshimiwa Shamsi Vuai Nahodha.

Baadhi
ya Wanachama wa SACCOS Ya Meli Nne jimbo la Mwanakwerekwe, Zanzibar
wakimshangalia Mke Wa Rais Mama Salma Kikwete wakati alipokuwa
akiwahutubia huko Chuo cha Karume, Zanzibar. Mama Kikwete ambaye pia ni
Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) alikuwa mgeni
rasmi kwenye ufunguzi wa Mkutano mkuu wa Tatu pamoja na viongozi wa
SACCOS hiyo.

Mke Wa
Rais Mama Salma Kikwete akiagana na Baadhi ya wananchama wa SACCOS ya
Meli Nne Mara baada ya kufungua Mkutano Mkuu wa Tatu wa SACCOS hiyo huko
Mwanakwerekwe, Zanzibar. Katika Hafla hiyo Mama Kikwete aliahidi
kuichangia shilingi Milioni Mbili na nusu 2.5m/-.
|