$2.4 Milioni kuipendezesha
Forodhani
28/04/2009

Bustani ya
Forodhani, Zanzibar (Forodhani Park) imerudishwa katika hali yake kama
ilivyokuwa wakati huo wa Sultan wa Zanzibar kwa msaada maalum wa Aga
Khan Trust for Culture (AKTC) kwa gharama ya dola 2.4m. Forodhani ni
sehemu ambayo hupendwa kutembelewa na wengi ambao ni wakazi wa Zanzibar
na wageni wanaotembelea Zanzibar. Ni sehemu mojawapo ya kivutio cha
matembezi ya Zanzibar.

Hii ndio
ilivyokuwa bustani ya Forodhani kabla ya matengenezo mapya.

Moja ya
nyumba ambazo zimepata kurejeshwa hali yake iliyokuwa kama zamani ni
nyumba iliyo pichani (The Old Dispensary).

The Old
Dispensary ikionekana pichani baada ya kufanyiwa ukarabati wa nguvu na
mradi maalum wa Aga Khan Trust for Culture. The Old Dispensary sasa
imepewa jina jipya na sasa inajulikana kama The Stone Town Cultural
Centre.

Bonyeza
kwenye mchoro wa Forodhani Park kwa kuona sehemu zilizoainishwa ambazo
zinafanyiwa ukarabati na kurudishwa hali yake kama ilivyokuwa zamani.
Zanzibar
ina nyumba nzuri za ajabu na za kihistoria ambazo zina-akisi utamaduni
wa Zanzibar na ufahari wa Tanzania nzima. Msaada wa Aga Khan Trust for
Culture (AKTC) umesaidia kuhifadhi nyumba na sehemu zenye kihistoria
Zanzibar na hii ni moja ya mfano wa kusaidia utamaduni wa Zanzibar na
Tanzania nzima kwa ujumla kutokupotea.
|