Sherehe za Muungano London
29/04/2009

Mheshimiwa Balozi wa
Tanzania nchini Uingereza, Mama Mwanaidi Senare Maajar, pamoja na Baba
Balozi, Bwana Sherif Maajar, waliwakaribisha Mh. Dr Lindiwe Mabuza,
Balozi wa Afrika ya Kusini nchini Uingereza, akifuatiwa na Balozi wa
Msumbiji, Mh. Antonio Gumede.

Mheshimiwa Balozi, Mama
Mwanaidi S. Maajar pamoja na Baba Balozi, wakimkaribisha Balozi wa
Botswana na vilevile ni Mkubwa wa Mabalozi wa Nchi za Afrika hapa
Uingereza, Mh. Roy Blackbeard.

Mabalozi, Wawakilishi,
Wanajumuiya za Watanzania na baadhi ya Wageni waalikwa wakisikiliza kwa
makini hotuba iliyotolewa na Mheshimiwa Balozi wa Tanzania, kwenye hafla
ya Muungano iliyofanyika Ubalozini, London.

Mheshimiwa Balozi, Mama
Mwanaidi S. Maajar, akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Viongozi
na Wawakilishi wa Jumuiya za Watanzania kwenye Sherehe za kuadhimisha
Miaka 45 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Toka kulia ni Bwana
Abubakar Faraj, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watanzania hapa Uingereza,
Bwana Katega, Muwakilishi wa Jumuiya ya Watanzania Birmingham, Bwana
Maina, Mwenyekiti wa chama cha CCM Reading, Bwana Jackson, Mwakilishi wa
Jumuiya ya Watanzania Birmingham, na Bwana Fredy (nyuma ya picha)
Mtanzania na Mtangazaji kutoka Idhaa ya Kiswahili ya BBC-London.

Mheshimiwa Balozi, akiwa
nje ya Westminster Abbey, London na Maofisa wengine wa Ubalozi, baada ya
kumalizika hafla ya Muungano ambayo huandaliwa kwa Kila Nchi Mwanachama
wa Commonwealth (mojawapo ni Tanzania) zinapofika siku kuu za nchi za
Mataifa ya Commonwealth. Kulia mwa picha ni Bwana David Nginilla, Bwana
Amos Msanjila, Mh. Balozi, Mama Mwanaidi. S. Maajar, Dada Caroline
Chipeta, na Bwana Clement Kiondo.
|