Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Mbagala na Majeruhi wa mabomu watembelewa

01/05/2009

Kikwete akiangali baadhi ya vipande na mabaki ya mabomu vilivyookotwa katika makazi ya watu wanaoishi karibu na kambi ya Jeshi la wananchi Mbagala jijini Dar es Salaam ambapo nyumba kadhaa ziliharibiwa vibaya na kwa mujibu wa taarifa ya polisi watu sita kupoteza maisha na 236 kujeruhiwa wakati ajali ilipotokea katika ghala la kuhifadhia silaha za kivita katika kambi hiyo. Wengine katika picha kutoka kushoto ni Mkuu wa usalama na utambuzi Jeshini Brigedia Jenerali Paul Meela, Naibu Waziri wa Ulinzi na jeshi la kujenga Taifa Emanuel Nchimbi, Mkuu wa majeshi ya Ulinzi na Usalama Jenerali Davis Mwamunyange na Inspekta Jenerali wa Jeshi la Polisi Said Mwema.

Makamu wa Rais Dk Ali Mohamed Shein akipata maelezo toka kwa Mkuu wa Kikosi cha Jeshi la Wananchi wa Tanzania Brigedia  Jenerali F. N. Ulomi, wakati alipotembelea Kambi ya Jeshi hilo eneo la Mbagala ambapo milipuko ya mabomu ilitokea jana na kusababisha madhara makubwa ya mali na watu.

Rais Kikwete akimpa pole mtoto Mariam Is-haq (8) aliyelazwa katika hospitali ya Wilaya ya Temeke baada ya kuathirika kwa mshtuko kutokana na ajali iliyotokea katika ghala la kuhifadhi silaha katika kambi ya jeshi huko Mbagala jijini Dar es Salaam. Pembeni aliyeketi na Mtoto Miriam ni mama yake Husna Suleiman mkazi wa Mtoni Mtongani, jijini Dar es Salaam.

Madaktari Bingwa katika Taasisi ya Mifupa ya Moi katika hospitali ya Taifa ya Muhimbil(kulia) wakimpa Rais Kikwete (kushoto aliyevaa mavazi maalum) maelezo ya mgonjwa aliyejeruhiwa vibaya na moja ya mabomu yaliyolipuka katika ajali iliyotokea katika ghala la kuhifadhia zana za kivita katika kambi ya jeshi la Wananchi wa Tanzania huko Mbagala, jijinji Dar es Salaam. Mgonjwa huyo amepoteza mguu wa kulia na amepoteza damu nyingi na anapumua kwa kutumia mashine maalum (Life Supporting Machine ). JK  alirejea jijini Dar es Salaam akitokea mjini Arusha ambapo alihudhuria mkutano wa wakuu wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki na kwenda huko moja kwa moja.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©