Polisi wapambana na
majambazi Dar es Salaam
08/05/2009

Mpambano
kati ya Polisi na majambazi waliovamia mtaa wa Swahili ulimalizika na
miili ya majambazi watatu kuuliwa hapo hapo na wengine watatu kujeruhiwa
vibaya.
Majambazi hao ambao wakati walipokuwa
wakirushiana risasi na Polisi,
walikuwa
wamebana karibu na gari iliopo kulia chini (pichani). mmoja wao alikuwa
amevaa mkanda wa risasi na alikuwa anamwaga njugu kama hana akili vizuri.

Wakati wa mpambano huo, baadhi ya watu
walithubutu kutoa pua wasipitwe na tukio la roho mkononi.

Mtaa wa Swahili ulikuwa katika hali ya
heka heka.

Raia na Polisi walikuwa makini na nafsi
zao wakati wa pambano hilo.

Lakini kila kitu kina mwisho wake. Mmoja
wa majambazi waliouwawa akionekana akitiwa nyuma ya gari la Polisi.

Heka heka hizo zilidumu kama dakika 45
mpaka Polisi kufikia kushinda.

Gari mojawapo ambayo inashukiwa ilikuwa ya
majambazi ikikaguliwa vilivyo na huku FFU wakiangalia kwa makini kabisa.

Askari wote wake kwa waume walikuwa na
kifaa, kuanzia bastola, bunduki, mabomu ya machozi, n.k.
|