Kura ya maoni visiwani
Komoro
19/05/2009

Huko visiwani Comoro tume ya uchaguzi
inasubiriwa kutoa matokeo rasmi ya uchaguzi wa kura ya maoni ya
kurekebisha katiba na sheria ya nchi uliomalizika hapo jana nchini humo.
Kurekebishwa kwa sheria hiyo kunatokana na
serikali ya muungano chini ya rais wake, Ahmed Abdallah Sambi, kuondoa
ule mfumo uliopo hivi sasa wa kuwepo kwa marais watatu wa visiwa vya
Ngazija, Nzuwani na Mwali na kuwa na bunge lao na hata mabaraza ya
mawaziri wa visiwa hivyo.
|