Kikwete atembelea Google -
Marekani
20/05/2009

Mchambuzi wa sera ya kampuni ya Google ya
Marekani, bwana Jake Hubert, akielezea mtandao wa kampuni hiyo
unavyofanya kazi kwa Rais Jakaya Kikwete aliyetembelea kampuni hiyo
katika eneo la Silicon Valley, San Jose, California.
Chuo kikuu maarufu cha Marekani na kampuni
kubwa tatu za teknolojia ya kompyuta zimekubali kuisaidia Tanzania
kujenga uwezo utakaoifikisha kwenye kilele cha kuwa nchi kiongozi katika
teknolojia hiyo Afrika. Chuo kikuu cha Stanford na kampuni ya Cisco,
Google na IBM, wametoa msimamo huo wakati walipompokea rais Kikwete na
kuzungumza naye katika ziara yake ya kikazi nchini Marekani.
|