Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Obama ahimiza kufungwa kwa Guantamo Bay

22/05/2009

Rais wa Marekani, Barack Obama, katika hotuba aliyotoa mjini Washington ameutetea mpango wake wa kutaka kuifunga jela ya Guantamo Bay kisiwani Cuba.

Obama alisema kuwa kuimarisha jela ya Guantamo Bay, imedhoofisha usalama wa taifa la Marekani (National Security).

Kwa mujibu wa mpango wa Obama, baadhi ya wafungwa 240 waliokuwepo Guantamo Bay, iliyopo Cuba, wahamishiwe Marekani katika jela zilizo na ulinzi mkali, baadhi yao watashtakiwa mahakamani Marekani, wengine watafikishwa mbele ya mahakama ya kijeshi na wengine wataachiwa huru kuambatana na amri zilizotolewa na mahakama.

Hapo awali, Obama alikataliwa kisiasa na Seneti kupewa dola milioni 80 kwa ajili ya mpango wa kuifunga jela ya Guantamo Bay.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©