Mufti Simba asafiri
kukaguliwa Afya yake
24/05/2009

Mufti wa Tanzania, Sheikh Issa Shaban
Simba, ameondoka nchini kwa ajili ya uchunguzi wa kawaida wa afya yake.
Taarifa ambazo zimepatikana kutoka kwa
waandishi wa habari zinasema kuwa, Mufti Simba ameondoka na kaimu katibu
mkuu wa Baraza Kuu la Waislamu wa Tanzania (BAKWATA), Sheikh Suleiman
Said.
Habari za kusafiri kwa Mufti
zilithibitishwa pia na Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Al-hajj Mussa
Salum, alipozungumza na waandishi wa habari.
Mufti amekuwa akisumbuliwa na matatizo ya
shinikizo la damu na kisukari kwa muda mrefu na mara kadhaa amekuwa
akisafiri kwenda India kwa uangalizi wa afya yake.
|