Sherehe za umoja wa Afrika
- Abu Dhabi, UAE
26/05/2009

Pichani juu na chini
Balozi wa Tanzania Mhe. Mohamed Maharage Juma akimkaribisha Mgeni rasmi
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje katika banda la Tanzania na
kumpatia vijarida juu ya fursa za uwekezaji Tanzania na zawadi za bidhaa
za Kitanzania ikiwemo asali, chai na kahawa.

Kivutio kikubwa kilikuwa
picha kubwa ya mlima Kilimanjaro ambapo wengi walipata somo kwamba upo
Tanzania na si kwingine popote.

Tarehe 25 Mei 2009 Balozi
za Kiafrika zilizopo Abu Dhabi, UAE (Umoja wa Falme za Kiarabu)
ziliadhimisha siku ya Umoja wa Afrika kwa semina juu ya fursa za
uwekezaji barani Afrika, maonyesho ya utamaduni na utalii wa nchi za
bara letu. Ubalozi wetu nchini humo ulishiriki vilivyo na wenzao.
|