Afisa Feki wa TRA abambwa
Dar es Salaam
28/05/2009

Mnamo
saa sita za mchana askari kanzu wa jiji la Dar es Salaam walimkamata
jamaa ambaye hujifanya Ofisa wa TRA katikati ya jiji la Dar; Afisa feki
huyo akionekana kushika kichwa pichani akijikinga na kipigo cha wenye
usongo na mali zao huku askari kanzu akijaribu kuzuia watu wasimkaribie
ili afikishwe sheriani kwa usalama.

Hapa akionekana kashikwa na askari kanzu
kuelekea garini la askari hao huku akishikwa mshiko wa unaojulikana aina
ya "No Smoking".

Afisa feki wa TRA akifikishwa ndani ya
gari kwa usalama na askari kanzu wa jiji la Dar es Salaam; Heko askari
kanzu wetu.
|