Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Jeetu Patel akiri na mabilioni ya pesa za EPA

31/05/2009

WAFANYABIASHARA Jayant Kumar maarufu kama Jeetu Patel na Devendra Patel wamekiri mahakamani kuwa kampuni ya Bencon Internatinal Limited inayodaiwa kujipatia fedha katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ni ya kwao. Wafanyabiashara hao walikiri hayo katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakati walipokuwa wakisomewa maelezo ya awali ya kesi yao.

Maelezo hayo yalisomwa na wakili wa serikali, Timon Vitalis mbele ya jopo la mahakimu watatu wanaosikiliza kesi hiyo Ruwaich Meela, Grace Mwakipesile na John Kahyoza. Washitakiwa hao walikiri kuwa wao ni kati ya wakurugenzi wa kampuni hiyo ambayo ilianzishwa hapa nchini Aprili 4 mwaka 2005. Pia Jeetu Patel na mshitakiwa mwingine Amit Nandy walikubali kuwa kampuni hiyo ilianzishwa hapa nchini Aprili 4 mwaka 2005 na kwamba wao ndio waliokwenda kufungua akaunti benki.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©