Mpango wa kuhifadhi Faru
wa Tanzania
04/06/2009

Faru akishushwa katika ndege akitokea
Jamuhuri ya Czeck ikiwa ni sehemu ya mpango maalum wa serikali
kuwarejesha nchini Faru ambao walikuwa wametoweka kinyume na sheria.
Faru huyo ni mmoja kati ya watatu toka Jamhuri ya Czech ambao
walirejeshwa juzi baada ya serikali kuwaomba kutokana na kuimarishwa
ulinzi ndani ya hifadhi.
Faru hao watahifadhiwa katika kituo maalum
cha mfuko wa hisani wa kulinda wanyama pori (WPTF) kilichopo ndani ya
hifadhi ya Mkomazi kwa muda wa miezi miwili kuzowea hali ya hewa ya
Tanzania na baadaye kuachiwa kuishi ndani ya hifadhi hiyo.
|