Mhanga wa mwisho wa meli
ya TITANIC afariki
05/06/2009

MILLVINA DEAN 1912
- 2009
Millvina Dean afariki
dunia akiwa na umri wa miaka 97, ni mmoja wa waliookoka na ndiye mhanga
wa mwisho katika wahanga waliosalimika katika ajali ya meli ya Titanic
iliyotokea tarehe 15 April 1912.

Millvina alikuwa na
umri wa wiki tisa tu wakati ajali hiyo ilipotokea baada ya kupiga mwamba
wa barafu katika bahari ya Atlantic ilipokuwa ikitokea Southampton, UK,
kuelekea New York, USA, na kusababisha watu 1,517 kufariki hapo hapo
kutokana na sababu moja wapo ya ukosefu wa majahazi ya kuokolea abiria.
Millvina amefariki
katika nyumba aliyokuwa akiangaliwa utu uzimani huko mjini Hampshire,
England, akiwa na umri wa miaka 97.
|