Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Jumuia mpya ya Watanzania UAE

06/06/2009

Balozi wa Tanzania nchini UAE, Mohamed Maharage Juma akimpongeza Mwenyekiti mpya wa jumuia ya Watanzania ambayo imeanzishwa na Watanzania nchini UAE, Bw Mohamed Shariff (kulia) na katikati ni Consul General, Ali Ahmed Saleh.

Mgeni wa heshima Mhe. Mohamed Maharage Juma, Balozi wa Tanzania nchini UAE (Umoja wa Falme za Kiarabu) aliyeongozana na Bw. Ali Ahmed Saleh Consul General wa Tanzania Dubai na Emirate za Kaskazini za UAE wakiwa pamoja na baadhi ya viongozi wapya wa jumuia mpya ya Watanzania (TAE) iliyozinduliwa nchini UAE. Mhe Balozi aliupongeza uongozi uliomaliza muda wake kwa kazi nzuri walioifanya ya kuasisi Jumuia na kuifikisha ilipo sasa na kuupa chanagamoto uongozi mpya kufanikisha malengo ya Jumuia na akaahidi kwamba Ofisi za Ubalozi na Consulate zitaendelea kusaidia shughuli za Jumuia kwa kadri ya uwezo wake.

Baada ya mkutano, Watanzania wanaoishi UAE walijumuika kupata mlo wa pamoja.

Viongozi Wakuu wapya ni kama wafuatao:

-Bw. Mohamed Shariff (Mwenyekiti)

-Bw. Mbarak Ahmed (Naibu Mwenyekiti)

-Bw. Shabir Damji (Katibu Mkuu)

-Eng. Issa Majid Magdi (Naibu Katibu Mkuu)

-Bw. Mohamed Manji (Mweka Hazina)

-Bw. Hassan Ally Abri (Naibu Mweka Hazina)

-Bw Abdulrahman Hassan (Mkurugenzi, Kurugenzi ya Jamii na Vijana)

-Bi Rahma Bukheti (Mkurugenzi Kurugenzi ya Wanawake)

-Bw Isaac Peter (Mkurugenzi Kurugenzi ya Mawasilano na Uhusiano)

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©