Madhehebu ya dini yapinga
kuondoshwa misamaha ya kodi
16/06/2009

SERIKALI inajitahidi katika mbio za
UCHUMI NA KUSAIDIA JAMII nchini. Pamoja na kuwa uchumi mwaka 2008
umeongezeka kwa asilimia 6.4 kwenye sekta ya uwekezaji wa mitaji ya
kigeni peke yake, serikali zinazungusha pesa hizo katika maeneo
mbalimbali ya kuendeleza nchi ikiwemo maeneo ya kusaidia jamii.
Lakini baadhi ya jumuia za NGOs na
madhehebu ya dini ambao wanatoa baadhi ya huduma kwa jamii
wamesikitishwa na wamepinga vikali matokeo ya bajeti ya Mwaka 2009/2010
ambayo imefuta misamaha ya kodi (VAT) kwa jumuia za NGOs na jumuia za
Kidini ambazo hapo awali jumuia hizo zilisamehewa kodi zake za VAT kwa
kuwapa mwanya jumuia hizo kutoa huduma za kijamii katika maeneo
mbalimbali na kupunguzia baadhi ya mizigo ya serikali.
Askofu Msaidizi wa Kanisa Katoliki Jimbo
Kuu la Dar es Salaam, Methodius Kilaini, amesema Kanisa limesikitishwa
na kusononeshwa mno na bajeti hiyo kwa vile inakatisha tamaa taasisi za
kidini ambazo zinatoa huduma njema, hususan makanisa.
|