Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Karume ahimiza Wakulima kushirikiana

20/06/2009

Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dk. Amani Abeid Karume amewahimiza wakulima wa Unguja na Pemba kushirikiana ili kuongeza uzalishaji wa chakula.

Rais Karume aliyasema hayo alipofanya ziara katika bonde la mpunga la Cheju lililopo Wilaya ya Kati, Mkoa wa Kusini Unguja na kuzindua uvunaji wa mpunga katika bonde hilo.

Aliwataka wakulima kuendelea kushirikiana kwa pamoja katika kuimarisha kilimo kwa kutambua kuwa uimarishaji wa kilimo utazidisha uzalishaji wa chakula na kuweza kukabiliana na tatizo la chakula lililopo ulimwenguni.

Akiwahutubia wakulima wa mpunga katika bonde hilo, Karume alisema Serikali iko katika juhudi za kuimarisha kilimo ikiwamo miundombinu.

Alisema juhudi za kuliimarisha bonde hilo zitaendelea kuchukuliwa kwa kuwa limewekwa katika Mpango maalum wa kilimo cha umwagiliaji maji katika visiwa vya Unguja na Pemba kwenye eneo lenye ukubwa wa hekta 8,500.

Karume aliahidi kupeleka jenereta kwenye bonde hilo mara taratibu za kuwekwa mabomba kumalizika.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©