Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Nasma Khamis afariki dunia

25/06/2009

FANI ya muziki wa taarabu nchini imepatwa na msiba wa kufariki mtunzi na mwimbaji mahiri, Nasma Khamis, umaarufu wake 'Kidogo'.

Nasma, 57, ambaye anakumbukwa kwa baadhi ya nyimbo zikiwamo, Mtu Mzima Ovyo, alifariki juzi jijini Dar es Salaam.

Kulingana na ndugu zake, Nasma alifariki saa sita usiku kwenye Hospitali ya Temeke alikokuwa amelazwa kutokana na kusumbuliwa na malaria.

Baba mdogo wa marehemu, Hamis Mohamed 'Kaniki' aliwaambia waandishi wa habari nyumbani kwake Kinondoni, Dar es Salaam ambako kumewekwa msiba huo kuwa Nasma alikuwa akisumbuliwa na shinikizo la damu mara kwa mara, lakini wiki iliyopita alilazimika kulazwa Temeke kutokana na hali yake kuwa mbaya na uchunguzi ulionyesha pia alikuwa na malaria.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©