Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Rubani afia angani

03/07/2009

Ndege ya Continental ikitokea Brussels kwenda New York ilibidi leo litue kwa dharura katika uwanja wa ndege wa Newark baada ya rubani kufariki dunia wakati wakiwa angani.

Ndege hiyo aina ya Boeing 777, ikiwa na abiria 247 ilitua salama mnamo saa kumi katika uwanja wa New Jersey, ambao ni mmoja kati ya viwanja vitatu vya jiji la New York.

Shirika la ndege la Continental katika taarifa yake limesema rubani huyo alikuwa na umri wa miaka 61 akiishi mjini Newark na alishafanya kazi kwa muda wa miaka 21. Hadi sasa sababu ya kifo cha rubani huyo haijajulikana.

Shirika la ndege la Continental ni la tano kwa ukubwa duniani na hutoa huduma kati ya Brussels na New York-Newark kila siku, na kuhudumia njia zipatazo 230 za Marekani, Latin na Amerika ya Kusini pamoja na Caribbean.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©