Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Maonyesho ya Sabasaba 2009

06/07/2009

Maonyesho ya sabasaba ya mwaka huu (2009) yamepiga hatua na sio kama ilivyokuwa miaka ya nyuma. Mandhari na majumba ya walioshiriki katika maonyesho hayo yametengenezwa kileo na hata milango ya kuingilia Sabasaba (pichani juu) imetengenezwa kileo na ya kupendeza na sio kama ilivyokuwa zamani.

Lango kuu la kuingilia kwenye maonyesho ya sabasaba ya mwaka 2009.

Vodacom Tanzania wamejipanga kisawasawa mwaka huu na harakati mbalimbali.

Sura mpya za aina ya mabanda zinaonekana safari hii.

Wachina ambao wana historia ya kushiriki katika maonyesho ya Sabasaba tangu enzi na enzi, mwaka huu wamechukua mtaa mzima kuonyesha hatua waliopiga ya uzalishaji.

Watani wa jadi na wao wako kamili kabisa.

Banda la wizara ya utalii na maliasili nao waliweka vitu vyote kuvutia watalii.

Njia ya kuelekea bustani ya wanyama pori ndani ya banda la wizara ya maliasili na utalii.

Inapendeza kwa wale ambao hawajapata kuona mali asili zao, wanapata muamko wa kuona mali asili ya nchi yao wakiwa jijini Dar es Salaam kwa njia ya usalama kabisa.

Watu mbalimbali wakiwa ndani ya bustani ya wanyama, wakimshangaa chatu mkubwa huku wakipewa maelezo mbalimbali kuhusiana na nyoka huyo mkubwa.

Pundamilia, moja ya wanyama wetu tunaojivunia nao Watanzania.

Sehemu ya mito asilia ikionyeshwa kwenye sehemu maalum iliyotengewa.

Sehemu ya shamba iliotegwa mizinga ya nyuki.

Pichani ni bustani ya miche ya miti ambayo ilitengewa sehemu yake maalum ya kuonyeshwa kwa waliozuru katika maonyesho ya Sabasaba ya mwaka huu 2009.

Maonyesho ya Sabasaba hutokea kila mwaka kuanzia tarehe 1 Julai mpaka kuadhimishwa kwake tarehe 7 Julai katika viwanja vya Mwalimu JK Nyerere, Kilwa Road, Dar es Salaam, Tanzania.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©