Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Kikwete acharuka, ataka Mabilioni yake yarejeshwe

08/07/2009

RAIS Jakaya Kikwete ametaka kurejeshwa kwa fedha alizozitoa kwa ajili ya mikopo ya kuwawezesha wananchi kuinua vipato vyao maarufu kama 'Mabilioni ya Kikwete' kama hazijafanyiwa kazi kama iliyokusudiwa.

Kauli hiyo ya Rais Kikwete alitoa wakati alipotembelea maonyesho ya 33 ya biashara ya kimataifa (BET) kwenye viwanja vya maonyesho vya kimataifa vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.

Kikwete alisema uamuzi huo unatokana na kutofanyiwa kazi kwa fedha hizo kama ilivyokusudiwa jambo ambalo analiamini kutokana na wananchi wake kulalamika.

"Fedha hizo ni zangu kama mmeshindwa kuzizungusha kwa wananchi naomba mzirudishe kwa kuwa nilizitoa kwa nia ya kuwasaidia wananchi wangu ili waweze kukabiliana na hali ngumu ya maisha," alisema Rais Kikwete.

Aliongeza kuwa lengo la kutoa fedha hizo ni kuwasaidia wananchi wake na kuleta tija kwa maendeleo ya nchi na sio watu wachache jambo ambalo limekwenda kinyume na utaratibu.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©