Mtambo wa gesi wazinduliwa
Dar es Salaam
15/07/2009

Waziri
wa Nishati na Madini, William Ngeleja (wa pili kulia) akikata utepe
ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa mtambo wa kushindilia gesi asilia
uliofanyika Ubungo jijini Dar es Salaam. Kulia ni Katibu Mkuu wa wizara
hiyo Ethur Mwakapugi na kushoto kwa waziri ni Meneja Mkuu wa PanAfrican
Energy (T) Ltd., Pierre Raillard.

Waziri
wa Nishati na Madini William Ngeleja akiweka gesi katika gari wakati wa
uzinduzi wa mtambo wa kushindilia gesi asilia uliofanyika Ubungo jijini
Dar es Salaam. Aliyesimama nyuma ya waziri ni Meneja Mkuu wa PanAfrican
Energy (T) Ltd Pierre Raillard.

Mfanyakazi wa PanAfrican Energy (T) LTD akimuonyesha Waziri wa Nishati
na Madini William Ngeleja (kushoto) jinsi ya kuweka gesi katika gari
maalum wakati wa uzinduzi wa mtambo wa kushindilia gesi asilia
uliofanyika Ubungo jijini Dar es Salaam.
|