Maonyesho ya historia ya
Soka (Soccer) nchini Tanzania
23/07/2009

Sehemu
ya majengo mapya ya makumbusho na nyumba ya utamaduni Dar es Salaam (ndipo
palipofanyika maonyesho ya historia ya soka nchini) zamani ikijulikana
kama makumbusho ya taifa, ambayo inafanyiwa ujenzi pamoja na ukarabati
wa nguvu kazi ambayo inategemewa kukamilika kabla ya mwisho wa mwaka huu
na kupafanya mahali hapa sio tu pa kutunzia historia bali pia sehemu ya
kukutana na kuburudika kwa tafrija mbalimbali na vyakula vya asili na
mengineyo.

Tangazo
la onesho la kumbukumbu ya soka nchini ambalo tarehe zake zimesogezwa
mbele kwa mwezi mzima kutokana na maombi ya wahudhuriaji na wapenzi wa
soka.

Mtaalamu
wa utafiti na mtunza historia katika makumbusho na nyumba ya utamaduni
B. Margreth M. Mapunda akionesha kitabu chenye historia ya mpira wa
miguu ambacho amekiandaa kwa ajili ya kuhifadhi kumbukumbu hiyo muhimu.
Kitabu hicho kinapatikana hapo makumbusho na nyumba ya utamaduni na kina
historia ndefu tokea enzi za Sunlight na Gossage cup, ikiwa ni pamoja na
wachezaji wa enzi hizo pamoja na viongozi.

Mmoja wa
waliohudhuria maonesho hayo akiangalia jezi namba 3 mgongoni iliyovaliwa
na beki hatari wa Taifa Stars enzi hizo Mohamed Chuma wa Mtwara aliyovaa
siku anastaafu kuchezea timu ya taifa mwaka 1976.

Mhudhuriaji wa maonesho ya historia ya soka akiangalia nyota wa zamani
wa soka nchini.

Sehemu
ya ukumbi wa maonesho wa makumbusho na nyumba ya utamaduni.

Wachezaji wa jimbo la nyanda za juu kusini mwaka 1955 katika kombe la
Sunlight, uwanja wa Ilala, siku hizi uwanja huo unajulikana kama uwanja
wa kumbukumbu ya Karume.

Viongozi
wetu walikuwa wapenzi wakubwa wa michezo. Simba wa vita Mzee Rashidi
Mfaume Kawawa akiiingia uwanjani kama refa katika mechi ya wabunge na
mabalozi miaka ya 70.

Mwalimu
Julius Nyerere akiwa na wachezaji na viongozi wa timu ya taifa
aliowakaribisha Ikulu baada ya kunyakua kombe la Gossage cup mwaka 1964.

Nahodha
wa timu ya taifa Mbwana Abushiri (Director Mbwana) akiwa kabebwa juu na
wenzie baada ya kunyakua kombe la Gossage cup mwaka 1964.

Timu ya
taifa wakiwa na kocha wao Millan Celebic (shoto juu) mwaka 1965.

Baadhi
ya marefa waandamizi miaka ya 1970 akiwemo Manyotto Ndimbo (wa sita
kulia) na Rajabu Marijani (wa nane kulia).
|