Idadi ya Watalii
yaongezeka Tanzania
27/07/2009

PAMOJA na mtikisiko wa uchumi unaoendelea
duniani, Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dk. Ladislaus
Komba amesema, tathmini ya awali ya biashara ya utalii nchini inaonyesha
kuwa idadi ya watalii inaongezeka hapa nchini kama ilivyopangwa.
Dk. Komba alisema, hali hiyo inaweza
kuendelea kuwa nzuri ikiwa huduma na miundombinu katika maeneo ya utalii
itaboreshwa na kutoa unafuu kwa watalii.
Alisema hayo alipokuwa akizungumza na
waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
Alisema tathmini inaonyesha kuwa idadi ya
watalii inazidi kuongezeka na kwamba kinachotakiwa kufanywa na serikali
kwa sasa, ni kuondoa baadhi ya kasoro za huduma kwenye sekta hiyo.
|