Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Tahadhari ya Majambazi

30/07/2009

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Afande Suleiman Kova alitoa tahadhari na kuwataka wote wanaohusika kukaa makini kuwa kuna kundi kubwa la majambazi wenye silaha kali, ambao wameingia Jijini Dar es salaam hivi karibuni.

Wahalifu hao ni pamoja na Wakenya ambao wana tabia ya kupora fedha katika taasisi kubwa kama mabenki, kampuni za mafuta na sehemu zenye biashara kubwa n.k.

Aliendelea kutoa onyo kamanda Kova na kusisitiza, watu hawa wana mbinu ya kula njama na watumishi wasiokuwa waaminifu. Ni muhimu mkafuatilia mienendo mbalimbali katika benki zenu na sehemu zilizotajwa hapo juu pamoja na kuimarisha usalama julisheni kwa message kupitia namba hii 0783034224 na kwa simu ya mdomo namba hii 0754034224 au 0787034224.

Namba hizi ni za mkuu wa Upelelezi Kanda maalum.
Lengo la maelezo si vitisho kwenu bali ni tahadhari muhimu,
inayofaa kuzingatiwa,
S. H. Kova - SACP
KAMANDA WA KANDA MAALUM
DAR ES SALAAM
 
   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©