Majambazi wavamia benki ya
NMB - Temeke
31/07/2009

Mkurugenzi wa Upeleleza wa Makosa ya Jinai afande Robert Manumba
akiongea na waandishi wa habari nje ya benki ya NMB, Temeke, Dar es
Salaam palipotokea tukio la kuvamiwa na majambazi. Waziri wa Mambo ya
Ndani, Mh. Lawrence Masha, Mkuu wa Polisi IGP Saidi Mwema na Mkuu wa
mkoa wa Dar es Salaam, Mh. William Lukuvi pia walikuja eneo la tukio
baadaye na kutembelea majeruhi waliolazwa hospitali ya Temeke iliyo
jirani na Benki hiyo.

Pichani
ni damu ya wafanyakazi wa katika kaunta ya benki ya NMB tawi la Temeke
ambapo majambazi yapatayo saba hivi yalivamia kwa mabomu ya mkono ambapo
baada ya kurusha mawili nje na kuua mlinzi wa kampuni binafsi aliyekuwa
getini, yakarusha risasi ndani na kujeruhi watu 13, ikiwa ni pamoja na
askari polisi wawili na kukomba takriban shilingi milioni 150 kabla ya
kutoroka. Majambazi hao walitoroka na Escudo na Prado zilizokuwa na
namba za 'SU' na 'STJ'.

Afande
wa FFU akiwa na guruneti moja ambalo halikulipuka katika uporaji wa
benki ya NMB tawi la Chang'ombe huko Temeke.

Wafanyakazi na wahusika mbalimbali
wakipigwa na butwaa baada ya tukio hilo kutokea.
Hii si
mara ya kwanza kutokea uporaji wa aina hii na umekuja siku moja tu baada
ya Kamanda wa kanda maalumu ya Dar es Salaam, Afande Suleiman Kova kutoa
tahadhari kwamba taarifa za kiintelejensia zao zinaonesha kuna kundi la
majambazi yenye silaha kali linataka kufanya uhalifu jijini. Tukio kama
hilo lilipata kutokea benki ya za Ubungo, Mwanga na Mbeya.
|