Duka la Gesi laripuka
Kigamboni
06/08/2009

Mwenye
duka la gesi pichani kulia akipiga taswira ya banda la kuuzia gesi
Kigamboni lililowaka moto na kutokea milipuko mikubwa. Mtu mmoja
amejeruhiwa na nyumba kama tano hivi zimeharibika kutokana na mripuko
huo ulioleta fadhaa kwa wakazi wa kigamboni na katikati ya jiji ambako
milio ilisikika kama mabomu. Vinginevyo, hakuna aliyefariki katika ajali
hiyo.
|