Fidia ya walioathirika na
mabomu Mbagala
13/08/2009

MAANDALIZI ya kuwalipa fidia wakazi wa
Mbagala walioathiriwa na mabomu yameanza.
Jumla ya Sh 8.5 bilioni zimetengwa kwa ajili ya
malipo ya fidia kwa wakazi ambao nyumba zao ziliathiriwa na milipuko ya
mabomu iliyotokea Aprili 29 kwenye ghala la silaha la kambi ya Jeshi la
Wananchi (JWTZ) iliyo Mbagala na kusababisha vifo vya zaidi ya watu 29.
Fedha hizo zitatumika kulipa fidia nyumba
9,259 zilizoharibiwa na mabomu hayo na ambazo zilihakikiwa na serikali.
|