Vodacom yazindua misaada
ya mwezi wa Ramadhan
26/08/2009

Mama Salma kikwete
akiwasili kwenye eneo la tukio mjini Bagamoyo tayari kuzindua kampeni ya
Vodacom Foundation ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ambapo pamoja na
kufuturisha sehemu mbalimbali nchini misaada kibao hutolewa.

Mama Salma Kikwete
akiwakabidhi vyakula watoto yatima ambao wanaishi katika mazingira
magumu. Msaada huo ulitolewa na Vodacom Foundation katika kampeni yao ya
mwezi mtukufu wa Ramadhan. Kulia kwa bi Salma, Mkuu wa Vodacom
Foundation Mwamvita Makamba, kushoto kwa bi Salma, Mkurugenzi mtendaji
wa Vodacom Tanzania Dietlof Mare, wilayani Bagamoyo.

Baadhi ya wanafunzi wa Madrasa wakiwa
katika hafla hiyo.

Mama Salma Kikwete
akimkabidhi vifaa vya charahani Mwenyekiti wa kikundi cha kina mama
wanaolea watoto yatima Bi. Muridhia Bakari. Msaada huo ulitolewa na
Vodacom Foundation katika kampeni yao ya mwezi mtukufu wa Ramadhan.
|