King's African Rifles
kuhakikiwa
28/08/2009

Serikali
imewataka askari wa King's African Rifles (KAR) waliopigana vita kuu ya
pili ya Dunia kuripoti katika ofisi za Mkuu wa mkoa au wilaya zao wakiwa
na vitambulisho au vielelezo husika kwa ajili ya uthibitisho wa
kutambuliwa.
Katika taarifa iliyotolewa hivi karibuni na Wizara ya Ulinzi na Jeshi la
kujenga Taifa yamehorodhesha majina ya askari wote waliopigana vita
hivyo vya mwaka 1939 hadi 1945.
Taarifa hiyo inasema kuwa orodha ya majina ya askari hao inapatikana
katika ofisi zote za mikoa na wilaya za Tanzania bara na Visiwani.
Mikoa hiyo ni Tanga, Arusha, Mjini Magharibi, Unguja na ofisi za wilaya
ya Tunduru, Songea, Nchingwea, Bunda, Serengeti, Bahi, Geita, Temeke,
Kisarawe, Ilala, Maswa, Babati, Morogoro, Mvomelo, Iringa, Kyela,
Singida na Dodoma mjini.
Wilaya nyingine ni Kishapu, Masasi, Shinyanga, Kilosa, Karangwe, Kondoa,
Tabora, Nzega, Mpanda, Kongwa, Biharamulo, Igunga, Misenyi, Muleba,
Handeni, Namtumbo, mkoa wa mjini Magharibi na Unguja, Wilaya ya
Magharibi na Kusini Unguja.
Pia katika orodha hiyo ya majina kuna majina ya askari wa King's African
Rifles (KAR) ambao hawajulikani maeneo waliyotoka.
Zoezi la uhakiki wa askari hao limeanza kufanyika tangu tarehe 15/8/2009
na litamalizika tarehe 30/10/2009.
|