Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) kuadhimisha miaka 45

30/08/2009

Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange akitoa maelezo kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya mambo ya nje Ulinzi na Usalama bwana Wilson Masilingi mara baada ya ufunguzi wa maadhimisho ya JWTZ kutimiza miaka 45. Mh. Masilingi alikuwa mgeni rasmi kwenye ufunguzi wa Maadhimisho hayo yaliyokuwa katika kikosi cha 603 cha jeshi eneo la Airwing, Ukonga jijini Dar es salaam. Kulia ni Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dk. Hussein Mwinyi na wa kwanza kushoto ni Naibu wake Dk. Emannuel Nchimbi.

Baadhi ya wananchi wakijitokeza kuangalia maonesho ya wiki ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kutimiza miaka 45 wakipata maelezo kuhusu silaha za kivita kutoka kwa wataalam wa Jeshi hilo.

Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya mambo ya nje, Ulinzi na Usalama Mh. Wilson Masilingi akipata ufafanuzi kutoka kwa Luten Kanali Anselum Bahati kuhusu bidhaa mbalimbali zinazotengenezwa na JWTZ kikosi cha Nyumbu wakati wa maonesho ya miaka 45 ya JWTZ. Kushoto ni Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange.

Wananchi wakijitokeza katika mabanda ya huduma za tiba kwenye maonyesho ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania kutimiza miaka 45.

Baadhi ya wananchi waliojitokeza kwenye maonyesho ya JWTZ kutimiza miaka 45 wakipata huduma za tiba na ushauri katika mabanda ya Maonyesho katika viwanja vya kikosi cha 603 cha Jeshi la Wananchi, Air wing, Ukonga jijini Dar es salaam.

Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya mambo ya nje Ulinzi na Usalama bwana Wilson Masilingi wakipata maelezo mara baada ya ufunguzi wa maonesho na maadhimisho ya JWTZ kutimiza miaka 45. Mh. Masilingi alikuwa mgeni rasmi kwenye ufunguzi wa Maadhimisho hayo yanayoendelea katika kikosi cha 603 cha jeshi eneo la Airwing, Ukonga jijini Dar es Salaam.

Askari wa kikosi cha anga katika maonesho hayo, wakiwakilisha kitengo chao cha anga huku kushoto ikionekana nembo yao ambayo imeandikwa UMOJA.

Wanafunzi wakiangalia baadhi ya silaha katika maonesho hayo.

Askari wenye silaha zenye nguvu za kutungua ndege katika maonesho.

Wananchi wakiangalia vifaa vya kijeshi kwenye maonesho hayo yaliyofanyika Air Wing, Ukonga mjini Dar es Salaam.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©