MV Magogoni mzigoni
01/09/2009

Kivuko cha MV Magogoni
kilichoundwa hapa Dar es Salaam kwa gharama ya Sh 8.5 bilioni na chenye
uwezo wa kubeba tani 500 wakiwemo abiria 2,000 na magari 60 kimeleta
wepesi kwa abiri wanaotumia kivuko hicho katika misafara yao ya kila
siku kivukoni.

Sehemu ya juu ya abiria inavyoonekana
kabla hawajaingia ndani.

Sehemu inayopakia magari ikionekana
imebeba magari na baadhi ya sehemu zikionekana bado ziko wazi.

Sehemu ya abiria ikionekana imechukua watu
kwa tanafasi na si kama ilivyokuwa zamani kubanana kama mshikaki. Kwa
mbaali kulia MV Alina ikionekana bado ikipiga mzigo kama kawaida.

MV Magogoni ikielekea Kigamboni.

MV Magogoni ikikata
maji kutoka Kigamboni.
Usafiri wa kivukoni umekuwa si wa shida tena kutokana na ujio wa MV
Magogoni toka rais JK kuzindua rasmi kivuko hicho mwezi Juni mwaka huu
na mchango mkubwa wa MV Alina kufanya kazi katika kivuko hicho.

MV Alina ikionekana inapiga mzigo kama
kawaida. Hali hii imesaidia kupunguza ajali ambazo zilikuwa zikitokea
mara kwa mara hapo awali katika kivuko hicho.
|