Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Mandy Juma apewa fursa kuendeleza kipaji cha Tennis

12/09/2009

Kijana Mandy akijidai na bendera ya taifa akiwa ubalozini jiini London alipofika kumsalimia Balozi wetu Uingereza Mh. Mwanaidi Maajar.

Mheshimiwa Mwanaidi Maajar akiwa na kijana Mandy ubalozini London.

Mandy akiwa pamoja na Baba yake Bwana Juma Rajabu Furaji na Bwana Hareen Wasantha, Mkurugenzi na ni Kocha wake.

Mandy akiwa kwenye picha ya pamoja na Mh. Balozi, wenyeji wake, baba mzazi, Kocha na Maofisa wa Ubalozini.

Mandy Juma Rajabu Furaji ni kijana mdogo wa Kitanzania aliyebahatika kupata ufadhili wa kuhudhuria chuo maalum cha kufundishia mchezo wa Tennis kiitwacho Tennis Avenue Academy hapa nchini Uingereza.

Kijana Mandy akiongozana na baba yake Bwana Juma Rajabu Furaji na wenyeji wao hapa Uingereza, Bwana na Bibi Mansela, walipata nafasi ya kutembelea Ofisi za Ubalozi wa Tanzania hapa nchini Uingereza, na kupokewa na Mheshimiwa Balozi, Mwanaidi Senare Maajar, pamoja na maofisa wengine wa Ubalozini hapo.

Baada ya kufanyiwa majaribio kadhaa na Walimu na Wataalamu wa Chuo hiko wamefurahishwa na wameridhia na kipaji, kiwango na umakini wa kijana Mandy na kumzawadia Scholarship (Ufadhili) kwa Umahili wake alionao kwenye mchezo huo maarufu wa Tennis.

Ikumbukwe kuwa mchezo huo wa Tennis ni ghali sana nchini Uingereza na kwenye nchi zilizoendelea. Mandy ataendelea na mafunzo yake ya Tennis chini ya Kocha wake na ambaye ni Mkurugenzi wa chuo hiko cha Tennis Avenue Academy kilichopo maeneo ya New Malden Surrey, Bwana Hareen Wasantha.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©