Mchango wa ZAIN katika
mwezi mtukufu wa Ramadhan Zanzibar
16/09/2009

Waziri wa Kazi, Vijana, Maendeleo ya
Wanawake na Watoto Zanzibar, Asha Abdallah Juma, akimkabidhi gunia la
mchele Talib Machano baada ya Madrasa yao ya Nuria kuibuka mshindi
katika shindano la kuhifadhi Qur'an. Hafla hiyo iliyodhaminiwa na Zain
Tanzania ilifanyika Hoteli ya Bwawani Zanzibar ambapo Zain pia
ilifuturisha watoto yatima. Katikati ni Mratibu wa Zain wa Kuendeleza
Biashara Zanzibar, Dominick Coy na kulia ni Mkurugenzi wa Chuchu Radio,
Yusuph Chuchu.
|