Mbuyu
04/10/2009

Mbuyu huu umepigwa picha katika mtaa
wa Mkungu Malofa, Chakechake, Pemba hivi karibuni.
Unakumbusha wengi na mengi mojawapo ni kwamba Ubuyu kwa sasa umekuwa ni
kitu kimojawapo ambacho ni zawadi kubwa ya tunu kupelekewa wanaoishi
ughaibuni, nje ya nchi.

Na unapotengenezwa kwa kutiwa rangi nyekundu na pilipili manga hupendwa
sana na si akinamama pekee sasa mpaka akinababa na watoto. Nasikia
ukiupata unaouzwa Jaws Corner, mjini Unguja ndio the best, (ni kweli
?...)
Wazungu karibuni ndio kwanza wameugundua na ubuyu umetambulika kwamba ni
Super fruit maana una Vitamin C nyingi sana kupita chungwa mara tano.
|