Wafanyakazi wa Air
Tanzania kupunguzwa
08/10/2009

SHIRIKA la Ndege la Air Tanzania (ATCL)
lipo katika hatua za mwisho za kukamilisha mchakato wa kupunguza zaidi
ya wafanyakazi wake 100 kwa lengo la kuboresha uendeshaji na huduma zake.
Shirika hilo liko kwenye hali mbaya ya
kifedha, sababu ya kupoteza biashara kubwa ya safari za ndege ndani na
nje ya nchi baada ya kupokonywa kwa muda hati yake ya usalama angani,
huku likielemewa na mzigo wa madeni, gharama za uendeshaji, ikiwa ni
pamoja na idadi kubwa ya wafanyakazi.
|