Barabara mpya kutoka
Jangwani mpaka Ubungo, Dar es Salaam
11/10/2009

Sehemu
ya barabara mpya inayokatiza Jangwani karibu na klabu ya Yanga kupitia
Kigogo, Mburahati, Mabibo na hatimaye Ubungo Maziwa ikiwa katika ujenzi
mojawapo wa kutanua na kuendeleza miundo mbinu ya usafiri jinini Dar es
Salaam.

Pia,
barabara hii ambayo inajengwa kwa kiwango cha lami, ni mojawapo ya
mikakati ya kupunguza msongamano wa foleni kwenye barabara ya miaka
nenda miaka rudi ya Morogoro rodi ambayo magari yote hutumia barabara
hiyo kama ndio lango kuu la jiji la Dar es Salaam kutokea na kuelekea
mikoani.

Hii pia ni mojawapo ya sehemu ya Jangwani
ambayo imekaa tayari kimchoro.

Hapa ni sehemu ya shule ya Loyola ambayo
inaonekana tayari ishakuwa tambarare.

Hapa ni sehemu ya Magomeni Mabibo ambayo
inaonekana tayari ishakuwa tambarare.
|