Stendi ya mabasi ya zamani
13/10/2009

Kwa
wakazi wa mji wa Dar es Salaam na wanaoujua mji wa Dar es Salaam bila ya
shaka wataijua sehemu hii iliyopo pichani juu. Hapa ndipo ilipokuwa
stendi ya zamani ya mabasi yaendayo kaskazini, mikoani hadi Nairobi na
Mombasa, karibu na posta ya mtaa wa Libya, maeneo ya Kisutu jijini Dar
es Salaam, kabla ya kituo hicho cha mabasi kuhamia Ubungo.
Ila
tangu stendi ihamishwe Ubungo miaka mingi iliyopita, sehemu hiyo
imeachwa tu patupu kwani sehemu hiyo ingeweza kujengwa gorofa la
kuegeshea magari tu ambalo lingechangia sana kuendesha uchumi wa Dar es
Salaam mjini ambapo watu wa kutoka sehemu mbalimbali za jiji na nje
wanakuja jijini kiuchumi, kisiasa, kielimu na mengineyo. Kwani sehemu
hii ilipo ni karibu na sehemu nyingi za mjini kwa mwendo wa miguu kutoka
hapa.
|