Kesi ya Liyumba kuanza
upya
22/10/2009

ALIYEKUWA Mkurugenzi wa
utumishi na utawala wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) Amatus Liyumba (pichani),ambaye
anakabiliwa na tuhuma za kutumia madaraka vibaya na kuisababishi
Serikali hasala ya mabilioni, ndiye aliyekuwa akiagiza kufanyika kwa
mabadiliko katika ujenzi wa majengo ya benki hiyo, yaliyoisababishia
Serikali kupata hasara.
Hayo yalielezwa jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, na shahidi
wa kwanza kutoka katika upande wa mashitaka wa kesi hiyo, ambayo Liyumba
nadaiwa kuisababishia Serikali hasara ya Sh Bilioni 221, kupitia ujenzi
wa majengo pacha ya BoT.
Mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo Edson Mkasimongwa, shahidi huyo
Seif Mohamed ambaye ni mchunguzi kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana
na Rushwa (TAKUKURU), alidai mahakamani hapo kuwa Liyumba ndiye
aliyekuwa na jukumu la kusimamia ujenzi wa jingo hilo.
Akiongozwa na Wakili wa Serikari Juma Ramadhani, Mohamed alidai kuwa
Liyumba alikuwa akitoa maagizo ya kwa aliyekuwa msimamizi wa wakandarasi
mkuu wa jengo hilo, juu ya mabadiliko ya jingo bila kupitia kwa bodi ya
benki hiyo.
Alidai kuwa Mkuu huyo wa wakandarasi, alikuwa akikubaliana na mabadiliko
hayo, na kuidhinisha kufanyika katika jingo, jambo ambalo ni kinyume na
makubaliano ya mkataba kati ya benki hiyo na kampuni ya ujenzi wa jengo
hilo.
Shahidi huyo alidai kuwa baadhi ya mabadiliko ambayo Liyumba aliyafanya,
yalisababisha gharama ya jingo hilo kufikia Dola za Marekani Milioni
357.7, badala ya kiwango kilichoidhinishwa hapo awali cha Dola za
Marekani Milioni 73.6.
Aliongeza kuwa katika mkataba ambao BoT iliingia na kampuni ya ujenzi wa
jengo hilo, bodi ya ya benki hiyo ilidhinisha gharama hizo za awali
kwasabau iliamini kuwa zingetosha kufanyika kwa ujenzi huo.
Kwa mujibu wa shahidi huyo, Liyumba alikuwa akipeleka mapendekezo ya
mabadiliko hayo kwa bodi ya benki hiyo, baada ya kuwa mabadiliko
kutendeka.
Naye Wakili Hillary Mkate ambaye anamtetea mshitakiwa huyo, alimuuliza
shahidi huyo maswali, ambapo Maojiano yao yalikuwa kama ifuatavyo;
Mkate: maelezo ya mwanzo yalidai kuwa bodi ya BoT iliruhusu mabadiliko
hayo kufanyika, je wewe unasemaje juu ya hilo?
Shahidi:hapana Liyumba alikuwa anatoa maagizo, ya mabadiliko na kabla
hata ya bodi kuidhinisha na mabadiliko yalikuwa yakifanywa.
Mkate:ni nani ambaye anamamlaka ya kubadili makubaliano yaliyokubaliwa
katika mkata?
Shahidi:ni bodi ya benki ndiyo iliyokuwa na uwezo huo, ingawa
haikuhusika katika mabadiliko hayo yaliyoisababishia Serikali hasara
Mkate:Imekuwaje Liyumba afanye mabadiliko hayo yanayohusisha mabilioni
ya fedha, bila kuihusisha bodi iliyokuwa na mamlaka ya kutoa fedha,
wakati yeye alikuwa si mjumbe wa bodi?
Shahidi:Liyumba alikuwa akiidhinisha kwanza mabadiko, kisha alikuwa
akirudi kwa bodi na kupeleka taarifa hiyo.
Mkatel:Na bodi hiyo ilikuwa ikisema nini juu ya hilo...???
Shahidi:Mara kadhaa bodi ilikuwa ikimkanya Liyumba kutokana na suala
hilo lakini aliendelea kufanya maamuzi bila kuishirikisha bodi.
Wakili Mkate aliendelea kuhoji suala hilo, huku akidai kuwa iweje bodi
hiyo ikubaliane na tabia ya Liyumba ya kufanya mabadiliko bila
kuishirikisha, na isimchukulie hatua?
Shahidi huyo alionekana kutokuwa na majibu ya maswali hayo.
Kesi hiyo iliahirishwa hadi leo, ambapo mahakama hiyo itasikiliza
ushahidi wa shahidi wa pili katika kesi hiyo.
|