Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Stendi ya Ubungo yakabidhiwa serikali

02/11/2009

KAMPUNI ya Smart Holdings, iliyokuwa ikisimamia uendeshaji wa Kituo Kikuu cha Mabasi ya kwenda mikoani cha Ubungo, Dar es Salaam, imekabidhi rasmi kituo hicho kwa serikali.

Makabidhiano hayo yalifanyika juzi usiku kwa mujibu wa Mkurugenzi mtendaji wa kampuni hiyo Hassan Khan, inafuatia kumalizika kwa mkataba wa miaka mitano ya kuendesha kituo hicho.

"Makabidhiana hayo yalifanyika usiku wa saa sita kwa sababu ya mkataba wetu ulikuwa unaishia siku ya 'wikiendi," alisema Khan.

Kwa mujibu wa mkurugenzi huyo, shughuli hizo zilishuhudiwa na Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam Alhaji Kingobi na viongozi wengine wa jiji.

Kampuni hiyo iliyoendesha kituo cha mabasi Ubungo tangu mwaka 2004, imekuwa ikihusishwa na mwanasiasa mkongwe hapa nchini Kingunge Ngombale Mwiru, lakini juzi Khan alikanusha kuwa mzee huyo na familia yake hawahusiani na kampuni hiyo.

Alisema kampuni hiyo inamilikiwa na yeye, Victor Mwiru na Peres Mwiru ambao hata hivyo, wakuwepo kwenye tukio la kukabidhiana kituo.

Khan alikuwa akijibu swali kuhusu wamiliki wa kampuni hiyo ambapo alisisitiza kuwa inamilikiwa kwa ubia.
 

Kampuni hii si ya kiongozi huyo anayetajwa tajwa wa watu, kampuni hii ni ushirikiano wa Hassan Khan, Victor Mwiru na Peres Mwiru, ambao wameungana na kuianzisha," alisema Khan.

Wakati wa ziara yake mwanzoni mwa mwaka huu katika kituo hicho Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, aliagiza kufanyika kwa uchunguzi wa hesabu za uendeshaji wa kituo hicho.

Hatua hiyo ilikuja baada ya baadhi ya wafanyabiashara kulalamikia ubadhirifu waliodai kuwa umekuwa ukinafanywa na viongozi wa kituo hicho chini ya Kampuni ya Smart Holdings.

Matokeo ya ukaguzi huo uliofanywa na ofisi ya Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali (CAG) yalionyesha kuwepo kwa ubadhirifu wa fedha katika uendeshaji wa kituo hicho.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©