Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

UMEME wa IPTL kuwashwa

05/11/2009

HATIMAYE kampuni ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL), imesema sasa inaweza kuwasha mitambo yake ya kuzalisha umeme baada ya serikali kuilipa kiwango walichokubaliana na kukamilika kwa matengenezo.

Serikali ilitangaza kuwa mitambo hiyo, inayoendeshwa kwa dizeli na yenye uwezo wa kuzalisha megawati 100, ingewashwa Novemba mosi baada ya Rais Jakaya Kikwete kuagiza “iwashwe mara moja, lakini baadhi ya mafundi wa kampuni hiyo waliiambia Mwananchi kuwa uwezekano wa kuiwasha tarehe hiyo ulikuwa ni mdogo na mitambo hiyo haijawashwa hadi sasa.

Jana, meneja utawala na uendeshaji wa IPTL, Venerabilis Jigge aliwaambia waandishi wa habari ofisini kwake Tegeta jijini Dar es salaam kuwa mitambo hiyo itawashwa wakati wowote wiki hii baada ya kukamilika kwa ukarabati na malipo hayo kwa ajili ya uendeshaji.

Meneja huyo hakutaja kiasi cha fedha kilichotolewa na serikali, lakini alisisitiza kuwa malipo hayo ni muhimu kwa uendeshaji wa mitambo hiyo.

Alieleza kuwa kuchelewa kwa malipo hayo kulisababisha ukarabati wa mitambo hiyo kuchelewa na hivyo kuchelewa kuiwasha.

Juzi serikali ilitulipa fedha tulizokuwa tumekubaliana. Tunategemea kuwasha mitambo wiki hii kwa kuwa fundi mkuu ametuthibitishia na tumeshakamilisha kila kitu ambacho kilikuwa kinaonyesha kuwa kinaweza kuwa kikwazo kwa kampuni katika uendeshaji mitambo hiyo, alisema Jigge.

Kwa mujibu wa meneja huyo, tayari IPTL imekabidhi fedha hiyo kwa kampuni ya Wartsila ambao wameingia mkataba wa miaka miwili na serikali kuendesha mitambo yake ya umeme.

Hivi sasa kazi ni kwa waendeshaji (Wartsila), kwani fedha tumeshawalipa jana(juzi) na mafuta yataanza kuingia leo (jana) jioni, alisema Jigge.

Jigge alisema ili kufanikisha kazi hiyo, tayari IPTL imeagiza tani 7,500 za mafuta kwa gharama ya Sh 7.5 bilioni.

Fundi mkuu wa kampuni ya Wartsila, Jaakko Kaihua alisema ukarabati wa mitambo hiyo unaendelea vizuri na kwamba, wakati wowote wiki hii itawashwa na kuzalisha umeme.

kama unavyosikia sasa mitambo inanguruma... tunaichemsha kwa sababu imekaa siku nyingi hivyo lazima tuichemshe,alisema Kaihua.

Alisema mafundi wa kuendesha mitambo hiyo walianza kuingia jana kutoka sehemu mbalimbali duniani na wataendelea kuja kadiri watakavyohitajika.

Siwezi kuahidi siku maalum ya kuanza kuwasha mitambo hii kwani bado tunaendelea na ukarabati lakini, hali si mbaya na ni matengenezo madogo tu yanayoendelea,alisema Kaihua.

Mitambo hiyo, ambayo inahusisha sehemu kumi ambazo kila moja ina uwezo wa kuzalisha megawati 10 kwa kila mmoja, ilifungwa nchini mwaka 1998.

Rais Kikwete aliagiza mitambo hiyo iwashwe mara moja baada ya wananchi na wafanyabiashara kumlilia kutaka aingilie kati kutatua tatizo kubwa la mgawo wa umeme unaondelea nchi nzima.

Kupungua kwa uzalishaji umeme kulikosababisha mgawo huo kumetokana na kuharibika kwa mitambo ya Songas inayotumia gesi asilia, na mingine kwenye mabwawa ya Kihansi na Hale na kupungua kwa kiwango cha maji katika mabwawa ya Kihansi na Pangani.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©