Mkutano wa kimataifa miaka
10 tangu Mwalimu kufariki
09/11/2009

Rais Mstaafu Mzee Ali Hassan Mwinyi
akiwasili Edinburgh, United Kingdom, kuhudhuria International High Level
Conference on Nyerere. Mkutano huo unatarajiwa kuwa wa siku mbili ambao
utazungumzia maisha ya Mwalimu Nyerere, mchango wake katika kujenga nchi
na mpaka kifo chake mwaka 1999. Mkutano huo unafanyika katika chuo kikuu
cha Edinburgh, Scotland, chuo ambacho alichosoma Mwalimu Nyerere kabla
ya kuwa Rais wa kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Balozi wa Tanzania nchini Uingereza (UK)
Mheshimiwa Mwanaidi Maajar (kushoto) akibadilishana mawazo na baadhi ya
wageni waliohudhuria mkutano huo mjini Edinburgh, Scotland.

Waziri wa mambo ya nchi za nje na
ushirikiano wa kimataifa, Mheshimiwa Bernard Membe (wa tatu Kushoto)
akiwa katika picha ya pamoja na wageni waliohudhuria mkutano huo wa
kutoka sehemu mbalimbali; wa kwanza kulia ni Mheshimiwa Mwanaidi Maajar.
Mheshimiwa Bernard Membe alimwakilisha rais Kikwete katika mkutano huo.
|